Mshindi wa Top Model Redd's Miss Tanzania 2012, Magdalena Roy akiwa katika pozi. Mshindi wa Top Model Redd's ...
Mshindi wa Top Model Redd's Miss Tanzania 2012, Magdalena Roy akiwa katika pozi.
Mshindi wa
Top Model Redd's Miss Tanzania 2012, Magdalena Roy (katikati anaepungia
mkono) akiwa na washiriki wenzake alioingia nao hatua ya tano bora
katika shindano lililomalizika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa
hoteli ya Naura Springs, Jijini Arusha.
Magdalena Roy (wa kwanza kushoto) wakati wa shindano hilo.
Na Mwandishi Wetu, Arusha
MISS Dar
City Center ambaye pia alishika nafasi ya pili katika shindano la Redd’s
Miss ilala, Magdalena Roy amefanikiwa kuingia 15 Bora ya Redd’s Miss
Tanzania baada ya usiku wa kuamkia leo kufanikiwa kutwaa taji la Top
Model.
Magdalena
anakuwa mshindi wa pili kuingia katika hatua hiyo, akiungana na Miss
Mbulu, Lucye Stephano ambaye wiki iliyopita alitwaa taji la Miss
Photogenic.
Katika
shindano la Top Model lililofanyika kwenye hoteli ya Naura Spring, mjini
hapa lilikuwa na upinzani mkali kutoka kwa washiriki wote wa Redd’s
Miss Tanzania.
Mbali na
Magdalena warembo wengine waliofanikiwa kuingia katika tano bora
walikuwa ni Mary Chizi (Ilala), Irene Veda (Lindi), Belinda Mbogo
(Dodoma) na Sina Revocatus (Elimu ya Juu).
Akizungumza
na Mtandao huu mjini hapa, Afisa Habari wa Kamati ya Miss Tanzania,
Haidan Ricco amesema warembo hao wataondoka kuelekea Tanga kwa ajili ya
kutembelea mapango ya Amboni, kabla ya kurejea Dar es Salaam.
Warembo
wapatao 30 wanawania taji la Redd’s Miss Tanzania, ambalo kwa sasa
linadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake
cha Redd’s Original.
Na globalpublishers