Wanawake wenye maumbo ya kati, ambao si wanene wala wembamba wamekuwa wakipendelea viatu virefu.PICHA|MAKTABA ...
Wanawake wenye maumbo ya kati, ambao si wanene wala wembamba wamekuwa wakipendelea viatu virefu.PICHA|MAKTABA
Na Ibrahim Bakari, Mwananchi
Posted Ijumaa,Decemba27 2013 saa 16:44 PM
Posted Ijumaa,Decemba27 2013 saa 16:44 PM
Kwa ufupi
Wengi, hasa wasichana wa kisasa. huamini kuwa viatu hivi vinawafaa, kumbe vina madhara kwao
‘Mchuchumio’ ama viatu vyenye visigino virefu,
ni mojawapo ya vitu vinavyopendwa na baadhi ya wanawake mbalimbali, si
katika Tanzania bali dunia nzima.
Wataalamu wanaeleza kuwa viatu hivi huharibu pingili za uti wa mgongo na huvunjavunja mifupa ya visigino.
Wanawake wenye maumbo ya kati, ambao si wanene wala wembamba wamekuwa wakipendelea viatu virefu.
Kwa kiasi kikubwa wasichana wafupi, wamekuwa wakipendelea kuvaa viatu virefu ili angalau na wao waonekane warefu.
Ashura Mgweno, mfanyakazi wa Kampuni ya Usafi
jijini Dar es Salaam, anasema: “Nimetumia viatu kwa muda mrefu, lakini
sasa sitaki kusikia viatu virefu. Mimi ni mfupi, nilikuwa navaa sana,
lakini sasa sitaki hata kuviona jinsi vilivyonitesa,” anasema.
Anasema kuwa viatu virefu muda wake ni miaka
mitatu, inaharibu visigino na misuli ya miguu na kutengeneza vigimbi
ambavyo baadaye husababisha maumivu makali.
Akizungumzia hili, Ruth Erasto ambaye anafanya
kazi katika ofisi moja jijini Dar es Salaam, anasema aliacha kuvaa
‘mchuchumio’ kwa maagizo ya daktari.
“Niligawa viatu vyangu vyote virefu baada ya
kupatwa na maumivu ya mgongo. Viatu virefu havilinganishi mwili wakati
wa kutembea na niliagizwa na daktari kuachana na viatu virefu...hiyo
ilitokana na mimi kuanza kupatwa na matatizo ya mgongo,” anasema.
Anasema kuwa alipatwa na matatizo hayo bila kufahamu, lakini baada ya kuchunguzwa, ndipo ikabainika kupatwa na matatizo hayo.
Mwanamama mwingine aliyepatwa na matatizo hayo,
Victoria, anasema kuwa inamlazimu kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili
(MNH) kila mara kwa ajili ya kuangaliwa maendeleo ya mgongo baada ya
kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu na kumletea athari hizo.
Victoria ambaye ni mfupi na mnene kiasi kwa
umbile, anasema kuwa pamoja na kupenda kuvaa viatu hivyo, hataki kusikia
habari zake.
“Nakuambia sina hamu na viatu hivi, acha kabisa,
nimekoma...nimekwenda Muhimbili hadi nimechoka, maumivu kuanzia kiuno
hadi mgongo,” anasema.